Yanga wanakwenda Nusu Fainali kwa faida ya ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza Jumapili iliyopita Nigeria, mabao ya mshambuliaji Mkongo, Fiston Kalala Mayele.
Yanga sasa itamenyana na Marumo Gallants ya Afrika Kusini ambayo imeitoa Pyramids ya Misri kwa jumla ya mabao 2-1, ikitoa sare ya 1-1 Cairo wiki iliyopita na kushinda 1-0 leo Phokeng, NW.
Mechi ya kwanza Yanga na Marumo Gallants itafanyika Dar es Salaam Mei 10 na marudiano yatafuatia Afrika Kusini Mei 17.
0 comments:
Post a Comment