• HABARI MPYA

    Saturday, April 15, 2023

    WASHINDI 100 MTOKO WA KIBINGWA WAWASILI DAR KUSHUHUDIA SIMBA NA YANGA


    HATIMAYE Kampeni ya Mtoko wa Kibingwa kupitia Kampuni ya Betika wawapokea washindi 100 kutoka mikoa yote Tanzania kwa ajili ya kutazama dabi kali afrika mashariki kati ya Simba na Yanga inayotarajiwa kukipiga kesho kwenye dimba la mkapa.
    Akizungumza mara baada ya kuwapokea washindi hao,Afisa Uhusiano wa BETIKA, Nelson Samweli amesema  Washindi hao  kutoka mikoa yote ya Tanzania Baada ya kufika watapelekwa kula bata pale kidimbwi leo na kesho watakaa VIAP A kushudia mechi ya Simba na Yanga watakaa VIP A.
    Hata hivyo,Samweli amesema Tangu wameanza kampeni ya mtoko wa kibingwa wamefanikiwa kuleta jumla washindi 400 kwa ndege kutoka mikoa yote Tanzania ambapo  Msimu wa 4 washindi  wa mtoko wa kibingwa walikuwa 50 sahivi mpaka 100.
    Kadhalika, Samweli amesema amewataka watanzania kuendelea kucheza kupitia BETIKA na kudai ukicheza unapata ushindi hapo hapo.
    kwa upande wao washindi wa BETIKA,Richard Mbewe ambaye ni miongoni mwa washindi wa mtoko kibingwa ameonesha furaha yake kuja Dar es Salaam.
    "Kweli nimeamini BETIKA hawana mbambamba ,katika maisha yangu sijawai kupanda ndege kupitia BETIKA nimepanda hatimaye nimekuja kutazama mechi ya watani ,najisikia furaha sana,nawashauri watanzania wenzangu tuendelee kucheza na BETIKA"Amesema Mbewe ambaye ni mmoja ya washindi wa promosheni ya mtoko wa kibingwa,ambapo washindi hao wataghalamiwa kila kitu wawepo hapa Dar es Salaam.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WASHINDI 100 MTOKO WA KIBINGWA WAWASILI DAR KUSHUHUDIA SIMBA NA YANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top