• HABARI MPYA

    Monday, April 24, 2023

    MANCHESTER UNITED WATINGA FAINALI KOMBE LA FA


    TIMU ya Manchester United imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la FA Cup England baada ya ushindi wa penalti 7-6 kufuatia sare ya 0-0 na Brighton & Hove Albion FC usiku wa Jumapili Uwanja wa Wembley Jijini London. 
    Ni Victor Lindelof aliyefunga penalti ya ushindi baada ya Solly March kukosa upande wa Brighton na sasa kikosi cha Erik ten Hag kitakutana na mahasimu, Manchester City katika Fainali Juni 3 hapo hapo Wembley.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANCHESTER UNITED WATINGA FAINALI KOMBE LA FA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top