KIKOSI cha Simba kinatarajiwa kuwasili Dar es Salaam kesho Saa 4:05 asubuhi kikitokea Morocco ambako jana kilitolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Safari ya Simba SC katika Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mara nyingine jana iliishia hatua ya Robo Fainali baada ya kutolewa na mabingwa watetezi, Wydad Club Athletic kwa penalti 4-3 Uwanja wa Mohamed V Jijini Casablanca, Morocco kufuatia sare ya jumla ya 1-1, kila timu ilishinda 1-0 nyumbani kwake.
0 comments:
Post a Comment