• HABARI MPYA

    Tuesday, April 18, 2023

    LIVERPOOL YAICHAPA LEEDS UNITED 6-1 ELLAND ROAD


    TIMU ya Liverpool imedhihirisha makali ya safu yake y ushambuliaji baada ya kuichapa Leeds United mabao 6-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Elland Road, Leeds, West Yorkshire.
    Mabao ya Liverpool yamefungwa na Cody Gakpo dakika ya 35, Mohamed Salah mawili dakika ya 39 na 64, Diogo Jota mawili pia dakika ya 52 na 73 na Darwin Nunez dakika ya 90, wakati la Leeds limefungwa na Luis Sinisterra dakika ya 47.
    Kwa ushindi huo, Liverpool inafikisha pointi 47 katika mchezo wa 30, ingawa inabaki nafasi ya nane, wakati Leeds yenye pointi 29 za mechi 31 inabaki nafasi ya 16.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YAICHAPA LEEDS UNITED 6-1 ELLAND ROAD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top