SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limewateua marefa wa Tanzania, Elly Sasii, Mohamed Mkono, Soud Lila na Ramadhan Kayoko kuchezesha mchezo wa kufuzu Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) baina ya Djibouti na Burundi.
Katika mechi hiyo itakayofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, Julai 29, mwaka huu, Kamisaa pia ni Mtanzania, Khalid Abdallah ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji TFF.
0 comments:
Post a Comment