• HABARI MPYA

    Wednesday, July 13, 2022

    AZAM FC YASAJILI KIPA MCOMORO ALIYECHEZA ULAYA


    KLABU ya Azam FC imemsajili kipa mkongwe wa kimataifa wa Comoro mzaliwa wa Ufaransa, Ali Ahamada ambaye amesaini mkataba wa miaka mitatu kutoka 
    Ahamada, mwenye umri wa miaka30, ni mmoja wa makipa wazoefu, aliyewahi kucheza klabu mbalimbali barani Ulaya, ikiwemo miamba ya Ufaransa, Toulouse, inayoshiriki Ligue 1.
    Brann ya Norway.
    Kabla ya hapo alicheza Toulouse kuanzia mwaka 2011 alikodaka jumla ya mechi 133 hadi anaondoka Ufaransa na kwenda Kayserispor ya Uturuki mwaka 2016 hadi 2019 alipohamia Kongsvinger ya Norway pia.
    Toulouse alianza kuchezea timu ya vijana mwaka 2009 akitokea Martigues iliyomuibua mwaka 2000 na kumkuza kisoka.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YASAJILI KIPA MCOMORO ALIYECHEZA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top