• HABARI MPYA

    Saturday, January 31, 2015

    MAN CITY CHUPUCHUPU KUZAMA KWA CHELSEA

    CHELSEA imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Manchester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Stamford Bridge, London.
    Loic Remy alianza kuwafungia The Blues dakika ya 41, kabla ya David Silva kuisawazishia City dakika nne baadaye.
    Kipindi cha pili milango ilikuwa migumu kwa pande mbili baina ya timu hizo mbili zinazoongoza mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England msimu huu.
    KIkosi cha Chelsea kilikuwa; Courtois, Ivanovic, Zouma, Terry, Azpilicueta; Ramires, Matic, Willian/Drogba dk80, Oscar/Loftus-Cheek dk93, Hazard na Remy/Cahill dk87.
    Man City; Hart, Sagna, Kompany, Demichelis, Clichy, Navas, Fernandinho, Fernando/Lampard dk77, Milner, Silva/Jovetic dk90 na Aguero/Dzeko dk84.
    Sergio Aguero celebrates with his team-mate following Silva's equaliser in the 45th minute
    Sergio Aguero akimpongeza mchezaji mwenzake David Silva baada ya kuisawazishia Man City dakika ya 45

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2934537/Chelsea-1-1-Manchester-City-Jose-Mourinho-s-remain-five-points-clear-league-leaders-claim-vital-point-Stamford-Bridge.html#ixzz3QQlB50Sm 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY CHUPUCHUPU KUZAMA KWA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top