BODI ya Ligi imefanya marekebisho ya kanuni kadhaa ikiwemo ya mchezo wa Ngao ya Jamii sasa kushirikisha timu nne.
Taarifa ya Bodi imesema timu tatu zilizomaliza nafasi ya juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara zitaungama na bingwa wa Azam Sports Federation Cup (ASFC) katika shindano hilo.
Lakini kama bingwa wa ASFC atakuwa miongoni mwa timu zilizomaliza nafasi tatu za juu kwenye Ligi Kuu, basi mshindi wa nne wa Ligi hiyo pia atashiriki Ngao ya Jamii.
0 comments:
Post a Comment