• HABARI MPYA

    Wednesday, August 17, 2022

    SIMBA SC YAMALIZIA HASIRA KWA GEITA, YAICHAPA 3-0


    WENYEJI. Simba SC wameanza vyema Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Geita Gold usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
    Mabao ya Simba SC leo yamefungwa na winga Mghana, Augustine Okrah dakika ya 37 na Wazambia, mshambuliaji, Moses Phiri dakika ya 61 na kiungo Clatous Chama kwa penalti dakika ya 81.
    Ushindi ni sawa na kupoza maumivu kwa mashabiki wa timu hiyo baada ya kuchapwa 2-1 na watani, Yanga katika mechi ya Ngao ya Jamii Jumamosi hapo hapo Mkapa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    1 comments:

    Idrisa rashidi akalama said... August 17, 2022 at 10:30 PM

    Yaani mwakauu yanga wajiandae kupokea kichapo wasione wameshinnda kwenye ngao ya isani sisi tumewaachia tu ''idrisa rashidi akalama nikiwa mnolela Lind

    Item Reviewed: SIMBA SC YAMALIZIA HASIRA KWA GEITA, YAICHAPA 3-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top