• HABARI MPYA

    Friday, August 19, 2022

    NAMUNGO FC YAICHAPA IHEFU 1-0 UHURU BAO LA LUSAJO


    BAO pekee la mshambuliaji Relliant Lusajo dakika ya 45 limeipa Namungo FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Ihefu SC jioni ya leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
    Ni ushindi wa kwanza kwa Namungo baada ya sare ya 2-2 na Mtibwa Sugar kwenye mechi ya kwanza na kipigo cha pili kwa Ihefu iliyorejea Ligi Kuu msimu huu baada ya kuchapwa 1-0 na Ruvu Shooting kwenye mechi ya kwanza.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAMUNGO FC YAICHAPA IHEFU 1-0 UHURU BAO LA LUSAJO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top