• HABARI MPYA

    Tuesday, August 09, 2022

    AZAM FC KUANZIA RAUNDI YA PILI, GEITA GOLD...


    TIMU ya Azam FC itaanzia Raundi ya Pili katika Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya mshindi kati ya Al Akhdar ya Libya na Al Ahly ya Khartoum nchini Sudan.
    Wawakilishi wengine wa Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, Geita Gold wataanzia Raundi ya Kwanza dhidi ya Hilal Al Sahil ya Sudan.
    Geita Gold wakifuzu mtihani huo watamenyana na Pyramids ya Misri katika Raundi ya Pili.
    Mechi za kwanza za Raundi ya kwanza zitachezwa kati ya Septemba 9 na 11 na marudiano Septembe 16 na 18wakati zaRaundi ya pili zitafuatia kati ya Oktoba 7 na 9 na marudiano Oktoba 14 na 16.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC KUANZIA RAUNDI YA PILI, GEITA GOLD... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top