WENYEJI, Singida Big Stars wameanza vyema Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons jioni ya leo Uwanja wa LITI, zamani Namfua, Singida.
Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliaji Mbrazil, Peterson Cruz dakika ya 36 na huo unakuwa mwanzo mzuri kwa timu hiyo ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba.
0 comments:
Post a Comment