• HABARI MPYA

    Sunday, August 14, 2022

    BRENTFORD YAITANDIKA MAN UNITED 4-0


    TIMU ya Manchester United chini ya kocha mpya, Mholanzi Erik ten Hag imepoteza mechi ya pili mfululizo kati ya mbili za mwanzo za msimu baada ya kuchapwa 4-0 jana na wenyeji, Brentford katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Gtech Community mjini Brentford, Middlesex.
    Mabao ya Brentford yamefungwa na Pelenda Joshua Tunga Dasilva dakika ya 10, Mathias Jensen dakika ya 18, Ben Mee dakika ya 30 na Bryan Mbeumo dakika ya 35.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BRENTFORD YAITANDIKA MAN UNITED 4-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top