KIUNGO wa ulinzi wa zamani wa Simba SC, Iddi Suleiman Kibode ‘Nyigu’ amefariki Dunia ya usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Muhimbili alipolazwa kwa matibabu.
Kibode, mdogo wa mshambuliaji wa zamani wa Simba, Madaraka Suleiman Kibode ‘Mzee wa Kiminyio’, alikuwemo kwenye kikosi cha Wekundu wa Msimbazi kilichofika Fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993.
Kibode katika picha hii ni wa pili kutoka kulia waliochuchumaa baada ya Edward Chumila (marehemu pia).
Mungu ampumzishe kwa amani.
0 comments:
Post a Comment