• HABARI MPYA

    Saturday, August 08, 2020

    JUVENTUS NAYO YATUPWA NJE KWA KURUHUSU BAO NYUMBANI

    Cristiano Ronaldo akisikitika baada ya Juventus kutolewa katika Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya licha ya kufunga mabao mawili dakika za 43 kwa penalti na 60 akimalizia pasi ya Federico Bernardeschi katika ushindi wa 2-1 kwenye mchezo wa marudiano usiku wa jana Uwanja wa Allianz, Torino. Bao la Lyon lilifungwa na Memphis Depay kwa penalti dakika ya 12 na kufanya sare ya jumla ya 2-2 na wageni kushinda 1-0 kwenye mchezo wa kwanza nyumbani, Ufaransa hivyo kusonga mbele kwa faida ya bao la ugenini na sasa itakutana na Manchester City iliyoitoa Real Madrid 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JUVENTUS NAYO YATUPWA NJE KWA KURUHUSU BAO NYUMBANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top