• HABARI MPYA

    Saturday, August 22, 2020

    UZINDUZI WA WIKI YA MWANANCHI, YANGA SC WATOA MISAADA YA VIFAA VYA MICHEZO SHULENI JIJINI DODOMA

    Na Mwandishi Wetu, DODOMA
    WADHAMINI wakuu wa mabingwa wa Kihistoria Tanzania, Kampuni ya SportPesa wametoa msaada wa mipira na vifaa vya Michezo kwa shule jijini Dodoma ikiwa ni mkakati wa kusaidia kukuza mchezo wa soka kwa vijana.
    "Mchezo wa soka ni ajira, sisi SportPesa tunaamini kwamba tukisadia vijana kukuza vipaji vyao tangu wakiwa chini tutatengeneza msingi na njia bora ya ajira yenye tija katika soka kwa vijana wetu hapo baadae," amesema Abbas Tarimba, Mkurugenzi wa Udhibiti na Uendeshaji wa Sportpesa Tanzania.
    Amesema kwa kupitia tukio la Uzinduzi wa Sportpesa Wiki ya Mwananchi, la klabu ya Yanga leo Kampuni hiyo itashirikiana vyema na Klabu kuhakikisha mchezo wa soka unaendelea kutengeneza mazingira bora ya ajira ya ndani na nje ya uwanja kwa wananchi.
    "SportPesa tutaendelea kurudisha sehemu ya faida tunayopata kwa jamii, kusaidia maendeleo yake katika nyanja mbalimbali, ikiwamo kwenye mchezo wenyewe wa mpira wa miguu," amesema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UZINDUZI WA WIKI YA MWANANCHI, YANGA SC WATOA MISAADA YA VIFAA VYA MICHEZO SHULENI JIJINI DODOMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top