KLABU ya Manchester City imeamua kusikiliza ofa za kuwauza wachezaji wake, Yaya Toure na Samir Nasri mwishoni mwa msimu, wakati mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya England wakitaka kuimarisha safu yao butu ya ulinzi.
Kocha wa City, Manuel Pellegrini yuko chini ya uangalizi maalum baada ya kipigo cha mabao 4-2 Jumapili kutoka kwa mahasimu na jirani zao, Manchester United.
Lakini wakati bodi ya City imeghairi kumtema kocha wao huyo, tayari uamuzi umefikiwa kusajili wachezaji bora wenye majina makubwa kwa ajili ya safu ya ulinzi, ambayo inaaminika ndiyo imemuangusha.
Manchester City imeamua kusikiliza ofa za kumuuza kiungo wa Ivory Coast, Yaya Toure mwishoni mwa msimu
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England, wapo tayari pia kumuuza Samir Nasri aondoke Uwanja wa Etihad


.png)
0 comments:
Post a Comment