• HABARI MPYA

    Thursday, April 30, 2015

    JOHN TERRY SASA NDIYE BEKI MFUNGAJI BORA KIHISTORIA LIGI KUU ENGLAND

    NAHODHA wa Chelsea, John Terry sasa ndiye mchezaji wa nafasi za ulinzi aliyefunga mabao mengi zaidi Ligi Kuu England baada ya Jumatano kufunga katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Leicester.
    Nahodha huyo wa zamani wa England alimtungua kipa Kasper Schmeichel Uwanja wa King Power jana kufunga bale la 38 tangu aanze kucheza Ligi Kuu.
    Bao hilo linamfanya Terry, ambaye amefunga kila msimu katika misimu 15 iliyopita Ligi Kuu kumfikia beki wa zamani wa Everton, David Unsworth. It was Terry's 38th Premier League goal during his career equalling the record for a defender

    MABEKI WATANO WAKALI WA MABAO KIHISTORIA ENGLAND 

    John Terry -  Mabao 38
    David Unsworth - Mabao 38
    Ian Harte - Mabao 28
    Leighton Baines - Mabao 26
    William Gallas - Mabao 25
    Kwa kuwa Terry bado yuko vizuri na anaendelea kucheza Chelsea kuna matumaini makubwa atafunga tena na kuwa beki mfungaji bora katika historia ya Ligi Kuu England.
    Unsworth, ambaye aliichezea timu ya taifa ya England pia, alikuwa mkali kwa guu lake la kushoto katika kufunga.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 41 sasa, ambaye mabao yake mengi alifunga akiwa na klabu hiyo ya Merseyside, Everton, alikuwa mtaalamu wa kupiga mikwaju ya penalti na mipira ya adhabu na Terry anafuata nyayo zake vizuri.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JOHN TERRY SASA NDIYE BEKI MFUNGAJI BORA KIHISTORIA LIGI KUU ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top