Toto Africans itashiriki tena Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu ujao |
Ofisa Habari wa Toto, Mariam Juma ameiambia BIN ZUBEIRY leo mjini Mwanza kwamba, Mkutano huo utaanza Saa 3:00 Asubuhi na Ajenda zitakuwa ni taarifa ya mapato na matumizi, kuhusu kujaza nafasi za Mwenyekiti na Wajumbe wawili waliojiuzulu na maandalizi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Mariam, mtangazaji wa Redio Metro FM mjini Mwanza, amesema kwamba wanachama wote wanatakiwa kufika mapema ili kushiriki Mkutano huo wa ustawi wa klabu yao.
“Tunaomba wanachama wote wa Toto wafike Mkutanoni, kwani Mkutano huu ndiyo dira ya timu yetu kwa msimu ujao katika Ligi Kuu,”amesema Mariam.
0 comments:
Post a Comment