• HABARI MPYA

    Monday, April 13, 2015

    BAADA YA KUWAPIGA NNE JANA, VAN GAAL AENDA KUJIRUSHA NA 'MADEMU' WA MAN CITY

    KOCHA wa Manchester United, Louis van Gaal jana amesherehekea ushindi wake wa 4-2 dhidi ya mahasimu, Manchester City kwa staili ya aina yake baada ya kupigwa picha akiwa na wachezaji wa timu ya wanawake ya Manchester City, Toni Duggan na Isobel Christiansen katika mgahawa.
    Duggan ameposti picha kwenye akaunti yake ya Instagram akiwa na Christiansen na Michelle Hinnigan wa Eveton katika mgahawa wa kichina wa Wing, kufuatia ushindi wa United wa 4-2 dhidi ya wapinzani wao wakubwa, City, na kuandika: "Heyyy Louis van G!!!! Nzuri kushea na wewe...... [sic].". Duggan baadaye akafuta posti hiyo.
    Wing ni sehemu ambayo wanasoka wanapenda kwenda mjini Manchester, miongoni mwao akiwa ni Nahodha wa England na United, Wayne Rooney, lakini wachezaji pekee wa City walionaswa nu Duggan na Christiansen.
    Louis van Gaal pictured with Manchester City women's players Toni Duggan (left) and Isobel Christiansen (far right), while they were joined by Everton's Michelle Hinnigan at Wing's restaurant
    Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal amepigwa picha akiwa na wachezaji wa timu ya wanawake ya Manchester City, Toni Duggan (kushoto) na Isobel Christiansen (kulia kabisa) na Michelle Hinnigan wa Everton katika mgahawa wa Wing kusherehekea ushindi wa 4-2 jana dhidi ya mahasimu wake hao katika Ligi Kuu ya England.
    Manchester United manager Louis van Gaal leaves Wing's restaurant after celebrating the win with friends
    Louis van Gaal akiondoka katika mgahawa wa Wing's baada ya kula bata na rafiki zake hao 
    Van Gaal was at the go-to restaurant for footballers and celebrities with his wife Truss and friends
    Van Gaal alikuwa katika mgahawa huo kufurahi pamoja na mkewe, Truss na rafiki zake 

    PICHA ZAIDI NENDA: 

    http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-3036546/Louis-van-Gaal-celebrates-Manchester-derby-win-restaurant-snapped-CITY-women-s-players-Juan-Mata-Daley-Blind-Ander-Herrera-hit-town-too.html#ixzz3XCcMVPDH 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BAADA YA KUWAPIGA NNE JANA, VAN GAAL AENDA KUJIRUSHA NA 'MADEMU' WA MAN CITY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top