// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SIR FERGUSON ATUA KWA HELIKOPTA UWANJANI KUISHUHUDIA MAN UNITED - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SIR FERGUSON ATUA KWA HELIKOPTA UWANJANI KUISHUHUDIA MAN UNITED - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, January 05, 2015

    SIR FERGUSON ATUA KWA HELIKOPTA UWANJANI KUISHUHUDIA MAN UNITED

    KOCHA wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson alihakikisha haukosi mchezo wa kwanza wa kocha Louis van Gaal wa Kombe la FA Cup baada ya kuchukua helikopta kwenda Somerset kuwashuhudia Mashetani Wekundu wakicheza.
    United imeinga timu ya Daraja la Kwanza, Yeovil Town mabao 2-0 Jumapili na Ferguson, aliyestaafu Mei mwaka 2013, alipaa kwa helikopta hadi Uwanja wa Huish Park na kutulia jukwaani.
    Akiwa amefungwa manbao 4-0 na MK Dons katika Raundi ya Pili ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Agosti mwaka jana na hana mashindano ya Ulaya msimu huu, mechi dhidi ya timu ya Gary Johnson inayosuasua ilikuwa ya pili nje ya Ligi Kuu.
    Sir Alex Ferguson's helicopter prepares to land near Yeovil Town's stadium Huish Park
    Helikopta ya Sir Alex Ferguson ikiwa angani tayari kutua Uwanja wa Yeovil Town, Huish Park
    Former Manchester United boss Ferguson waves for the cameras after touching down in Yeovil
    Kocha wa zamani wa Manchester United, Ferguson akiwapungia mikono mashabiki baada ya kutua mjini Yeovil
    Ferguson (left) won five FA Cups during his 26-and-a-half years as manager of Manchester United
    Ferguson (kushoto) alitwaa mataji matano ya Kombe la FA katika miaka yake 26 na nusu ya kuiongoza Manchester United
    Ferguson watches United beat Yeovil 2-0 at Huish Park as Sir Bobby Charlton (top left) also looks on
    Ferguson akiishuhudia United ikiipiga Yeovil 2-0 Uwanja wa Huish Park huku Sir Bobby Charlton (juu kushoto) pia akiangalia
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIR FERGUSON ATUA KWA HELIKOPTA UWANJANI KUISHUHUDIA MAN UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top