// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); DAVID MOYES AWAKUNG'UTA BARCELONA LA LIGA NA MESSI, SUAREZ NA NEYMAR WAO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE DAVID MOYES AWAKUNG'UTA BARCELONA LA LIGA NA MESSI, SUAREZ NA NEYMAR WAO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, January 05, 2015

    DAVID MOYES AWAKUNG'UTA BARCELONA LA LIGA NA MESSI, SUAREZ NA NEYMAR WAO

    KOCHA wa zamani wa Manchester United, David Moyes usiku huu ameiongoza timu yake mpya, Real Sociedad kuiangusha Barcelona kwa bao 1-0 katika La Liga Uwanja wa Aneota. 
    Barcelona imepoteza nafasi nzuri ya kupanda kileleni mwa La Liga kwa kipigo hicho na kocha Luis Enrique atajilaumu kwa kuwaanzishia benchi wachezaji wake nyota wakiwemo Lionel Messi, Neymar na Gerard Pique.
    Ushindi huo wa kikosi cha David Moyes ni muendelezo wa ubabe dhidi ya vigogo, baada ya awali kuwafunga Real Madrid na Atletico Madrid Uwanja wa Anoeta msimu huu.
    Beki wa Barca, Jordi Alba alijifunga mapema dakika ya pili tu kuipatia ushindi huo timu ya Moyes. Mapema katika mchezo uliotangulia, Real Madrid ilifungwa mabao 2-1 na Valencia Uwanja wa Mestalla, licha ya Cristiano Ronaldo kutangulia kufunga.
    Kikosi cha Real Sociedad kilikuwa; C. Martinez, Ansotegi, I. Martinez, De La Bella, Markel, Granero, Xabi Prieto, Canales, Castro/Finnbogason na Vela.
    Barcelona; Bravo, Montoya, Mascherano, Mathieu/Alves, Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Munir/Messi, Suarez na Pedro/Neymar.
    Luis Suarez (left) looks on as Real Sociedad players celebrate taking an early lead as La Liga resumed after the winter break
    Luis Suarez (kushoto) akiwaangalia wachezaji wa Real Sociedad wakishangilia bao lao la mapema lililodumu hadi mwisho mwa mchezo huo wa La Liga
    David Moyes' side had previously beaten Atletico Madrid and Real Madrid at the Anoeta Stadium this season
    Kocha David Moyes akiwa kazini Uwanja wa Anoeta dhidi ya Barca

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2896419/Real-Sociedad-1-0-Barcelona-David-Moyes-giant-killers-prevent-Lionel-Messi-taking-spot-La-Liga.html#ixzz3NtTuNopf 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DAVID MOYES AWAKUNG'UTA BARCELONA LA LIGA NA MESSI, SUAREZ NA NEYMAR WAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top