• HABARI MPYA

    Thursday, May 11, 2023

    ASEC MIMOSA YABANWA NYUMBANI, 0-0 NA USM ALGER


    WENYEJI, ASEC Mimosa wamelazimishwa sare ya bila kufungana na USM Alger
    katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika usiku wa jana Uwanja wa Bouaké, Bouaké nchini Ivory Coast.
    Timu hizo zitarudiana Mei 17 Uwanja wa Julai 5 1962 Jijini Algiers na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla katí ya Yanga ya Tanzania na Marumo Gallants ya Afrika Kusini.
    Mechi ya kwanza baina ya timu hizo, Yanga ilishinda 2-0 bila Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam na sasa zitarudiana Mei 17 Afrika Kusini. Fainali zitapigwa Mei 28 na Juni 3 nyumbani na ugenini pia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ASEC MIMOSA YABANWA NYUMBANI, 0-0 NA USM ALGER Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top