• HABARI MPYA

    Tuesday, May 16, 2023

    UONGOZI MARUMO GALLANTS WAKANUSHA KUDAIWA NA WACHEZAJI

    UONGOZI wa Marumo Gallants umekanusha taarifa kwamba unadaiwa posho na wachezaji wake na kusema hali ni shwari wameelekeza nguvu zao kwenye mchezo wao wa kesho dhidi ya Yanga.
    Marumo Gallants watakuwa wenyeji wa Yanga kesho katika mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Royal Bafokeng mjini, Phokeng Jijini Rustenburg.
    Wanahitaji ushindi wa kuanzia mabao 3-0 ili kwenda Fainali kutokana na kufungwa 2-0 na Yanga kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UONGOZI MARUMO GALLANTS WAKANUSHA KUDAIWA NA WACHEZAJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top