TIMU ya Nottingham Forest imetoka nyuma na kupata sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji, Chelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Mabao ya Nottingham Forest yamefungwa na mshambuliaji wake wa Kimataifa wa Nigeria, Taiwo Michael Awoniyi yote mawili, dakika ya 13 na 62, wakati ya Chelsea yamefungwa na nyota wa England, Raheem Sterling yote pia, dakika ya 51 na 58.
Kwa sare huyo Chelsea inafikisha pointi 43 katika mchezo wa 35 nafasi ya 11 na Nottingham Forest inafikisha pointi 34 za mechi 36 nafasi ya 16.
0 comments:
Post a Comment