• HABARI MPYA

    Monday, August 23, 2021

    MCUBA AMSHINDA PACQUIAO KWA POINTI

    BONDIA mkongwe, Manny Pacquiao jana amepigwa kwa pointi na Mcuba, Yordenis Ugas katika pambano ambalo linaweza likawa la mwisho kwake lililofanyika ukumbi wa T-Mobile Arena, Jijini Las Vegas, Marekani kuwania ubingwa wa WBA uzito wa Super Welter.

    Lakini Mfilipino huyo atakayetimiza miaka 43 baadaye mwaka huu hakutaka kusema atastaafu au la baada ya pambano hilo majaji wawili wakitoa pointi 116-112 kwa Ugas, na wa tatu 115-113.

    Yordenis Ugas mwenye umri wa miaka 35 alipewa nafasi ya kupigana na Pacquiao wiki iliyopita tu baada ya mpinzani wa awali, Errol Spence Jr kujitoa kufuatia kuumia mazoezini.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MCUBA AMSHINDA PACQUIAO KWA POINTI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top