• HABARI MPYA

    Sunday, March 05, 2023

    MBEYA CITY YAWATUPA NJE KAGERA SUGAR ASFC


    BAO la mkwaju wa penalti la Richardson Ng’odya dakika ya 60 limeipa Mbeya City ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba leo.
    Kwa ushindi huo, Mbeya City inakwenda hatua ya Robo Fainali ya michuano hiyo ikiungana na mabingwa watetezi, Yanga, Simba, Geita Gold, Ihefu SC, Mtibwa Sugar na Singida Big Stars.
    Orodha ya timu za Robo Fainali itakamilika baada ya mchezo wa mwisho wa Hatua ya 16 Bora baina ya wenyeji, Azam FC na Mapinduzi ya Mwanza usiku wa leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MBEYA CITY YAWATUPA NJE KAGERA SUGAR ASFC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top