• HABARI MPYA

    Wednesday, March 29, 2023

    SIMBA WAKWAMA ARUSHA WAKIENDA MOROCCO NDEGE YAPATA HITILAFU


    MSAFARA wa kwanza wa Simba ulioondoka leo jioni Dar es Salaam kwenda Morocco kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Afrika dhdi ya wenyeji Raja Casablanca Aprili 1 umelazimika kuishia Arusha.
    Afisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally amesema hiyo imetokana na ndege waliyokuwa wanasafiria kupata hitilafu baada ya kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jioni ya leo.
    Sasa msafara huo utaunganisha safari mapema kesho asubuhi kwenda Morocco.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA WAKWAMA ARUSHA WAKIENDA MOROCCO NDEGE YAPATA HITILAFU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top