• HABARI MPYA

    Friday, March 24, 2023

    RAIS SAMIA ANUNUA TIKETI 2000, WAZIRI MKUU 2000 MECHI YA TAIFA STARS NA UGANDA


    RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amenunua tiketi 2,000 kwa ajili ya kampeni ya kuhamasisha mashabiki kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo dhidi ya Uganda.
    Taifa Stars leo wanamenyana na The Cranes Uwanja wa Suez Canal Jijini Ismailia katika mchezo wa Kundi F kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani nchini Ivory Coast na timu hizo zitarudiana Jumanne Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam
    Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa naye ameshiriki katika Kampeni hiyo kwa kununua tiketi 2000 kwa ajili ya mashabiki.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RAIS SAMIA ANUNUA TIKETI 2000, WAZIRI MKUU 2000 MECHI YA TAIFA STARS NA UGANDA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top