• HABARI MPYA

    Saturday, March 25, 2023

    MAHODHA MPYA MBAPPE APIGA MBILI UFARANSA YAICHAPA UHOLANZI 4-0


    NAHODHA mpya, Kylian Mbappe usiku wa jana amefunga mabao mawili Stade de France mjini Saint-Denis kuiwezesha Ufaransa kuitandika Uholanzi 4-0 katika mchezo wa kwanza wa Kundi B kufuzu Euro 2024 Ujerumani.
    Mbappe ambaye pia ni Nahodha wa Paris Saint-Germain alifunga mabao yake dakika ya 21 na 88, wakati mabao mengine yamefungwa na Antoine Griezmann dakika ya pili na Dayot Upamecano dakika ya nane.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAHODHA MPYA MBAPPE APIGA MBILI UFARANSA YAICHAPA UHOLANZI 4-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top