TIMU ya Manchester City imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la FA England baada ya ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Burnley jana Uwanja wa Etihad Jijini Manchester.
Mabao ya Manchester City yamefungwa na Erling Haaland matatu dakika za 42, 35 na 59 na sasa anafikisha mabao 42 jumla msimu huu, wakati mengine yamefungwa na Julian Alvarez dakika ya 62 na 73 na Cole Palmer dakika ya 68.
0 comments:
Post a Comment