ROBO Fainali za Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) zitaanza Aprili 2 kwa mchezo kati ya Singida Big Stars na Mbeya City Uwanja wa LITI mjini Singida.
Robo Fainali ya pili itafuatia Aprili 3 kwa mchezo kati ya Azam FC na Mtibwa Sugar Uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Robo Fainali ya tatu ni Aprili 7 baina ya Simba SC na Ihefu Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, wakati mabingwa watetezi, Yanga SC watakamilisha ngwe hiyo kwa kumenyanana na Geita Gold Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Aprili 8.
0 comments:
Post a Comment