• HABARI MPYA

    Friday, March 17, 2023

    NI REAL MADRID NA CHELSEA ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA


    MABINGWA watetezi, 
    Real Madrid watamenyana na mabingwa wa mwaka 2021, Chelsea kwenye Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wakati Manchester City watacheza na Bayern Munich
    Katika droo ya Robo Fainali iliyopangwa leo, Benfica ya Ureno itamenyana na Inter Milan, wakati AC Milan watacheza na Napoli, zote za Italia.
    Mshindi kati ya Real Madrid na Chelsea atakutana na mshindi kati ya Man City na Bayern Munich katika Nusu Fainali, wakati  mshindi kati ya Benfica na Inter Milan atamenyana na mshindi kati ya AC Milan na Napoli.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI REAL MADRID NA CHELSEA ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top