MABINGWA watetezi, Real Madrid watamenyana na mabingwa wa mwaka 2021, Chelsea kwenye Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wakati Manchester City watacheza na Bayern Munich.
Katika droo ya Robo Fainali iliyopangwa leo, Benfica ya Ureno itamenyana na Inter Milan, wakati AC Milan watacheza na Napoli, zote za Italia.
Mshindi kati ya Real Madrid na Chelsea atakutana na mshindi kati ya Man City na Bayern Munich katika Nusu Fainali, wakati mshindi kati ya Benfica na Inter Milan atamenyana na mshindi kati ya AC Milan na Napoli.
0 comments:
Post a Comment