• HABARI MPYA

    Tuesday, April 14, 2015

    MTIBWA SUGAR NA PRISONS ‘BONGE LA VITA’ KUIKATAA DARAJA LA KWANZA KESHO MANUNGU

    Prisons wanashika nafasi ya pili kutoka mkiani
    LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea kesho jumatano katika viwanja viwili nchini, jijini Tanga wenyeji Maafande wa Mgambo Shooting watawakaribisha timu ya Azam FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
    Mjini Morogoro wakata miwa wa Mtibwa Sugar watakua wenyeji wa maafande wa jeshi la Magereza nchini timu ya Tanzania Prisons kutoka Mbeya, mchezo utakaopigwa katika dimba la Manungu Turiani.
    Azam FC inahitaji ushindi kesho ili kufufua matumaini ya kutetea ubingwa wake, baada ya sare mbili mfululizo 1-1 zote, dhidi ya Mtibwa Sugar na Mbeya City, ambazo zimewafanya wazidiwe pointi nane na vinara, Yanga SC (46-38).          
    Mtibwa Sugar nao wanahitaji ushindi katika mchezo huo, kama ilivyo kwa Prisons ili kujiondoa katika mazingira ya kushuka daraja. Mtibwa ina pointi 24 za mechi 21, ikiwa inashika nafasi ya 11, wakati Prisons yenye pointi 21 za mechi 21, inashika nafasi ya 13 katika ligi ya timu 14.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTIBWA SUGAR NA PRISONS ‘BONGE LA VITA’ KUIKATAA DARAJA LA KWANZA KESHO MANUNGU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top