Jamie Vardy akishangilia baada ya kuifungia bao la kusawazsisha Leicester City dakika ya 84 ikitoa sare ya 1-1 na Arsenal iliyotangulia kwa bao la Pierre-Emerick Aubameyang dakika ya 21 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa jana Uwanja wa Emirates. Arsenal ilimaliza pungufu baada ya Eddie Nketiah kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 74, dakika nne tu tangu aingie kuchukua nafasi ya Alexandre Lacazette. Leicester inafikisha pointi 59 baada ya sare hiyo katika mchezo wa 34 na sasa inashuka hadi nafasi ya nne ikizidiwa pointi moja na Chelsea, wakati Arsenal inayofikisha pointi 50 baada ya kucheza mechi 34 pia inabaki nafasi ya saba PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Travis Kelce gives abrupt answer to question about Chiefs locker room
before Texans playoff showdown
-
The Kansas City Chiefs have the chance to do something that no team - not
the Cowboys, not the Steelers, not even the Patrtiots - has ever done: win
three ...
46 minutes ago
0 comments:
Post a Comment