Raheem Sterling usiku wa jana amefunga mabao mawili dakika za 31 na 40 Manchester City ikiichapa Watford 4-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England, mabao mengine yakifungwa na Phil Foden dakika ya 63 na Aymeric Laporte dakika ya 66 Uwanja wa Vicarage Road. Man City inafikisha pointi 78 baada ya ushindi huo kwenye mchezo wa 37, ingawa inabaki nafasi ya pilo nyuma ya mabingwa tayari, Liverpool wenye pointi 93 za mechi 36, wakati Watford inayobaki na pointi zake 34 baada ya mechi 37 pia, inashuka kwa nafasi moja hadi ya 18 sasa ikiwa hatarini zaidi kushuka daraja PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Watch: Lille midfielder Ethan Mbappe shown red card for ugly elbow
-
Ethan Mbappé was shown a red card in Lille's Champions League match against
Real Betis on Tuesday.
4 days ago



.png)
0 comments:
Post a Comment