• HABARI MPYA

    Tuesday, September 03, 2019

    TAIFA STARS WALIVYOONDOKA LEO DAR KUIFUATA BURUNDI KWA MECHI YA KUFUZU KOMBE LA DUNIA KESHO

    Beki Kelvin Yondan akiwaongoza wachezaji wenzake wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kuingia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) mjini Dar es Salaam kwa safari ya Bujumbura nchini Burundi leo asubuhi
    Taifa Stars inakwenda Bujumbura kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia Qatar 2022
    Kipa Juma Kaseja akiingia JNIA kwenda Bujumbura kwa ajili ya mchezo ambao utafanyika kesho
    Timu hizo zitarudiana Jumapili Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam na mshindi wa jumla atapangwa katika moja ya makundi 10 kuanza rasmi mbio za Qatar 2022
    Kiungo Mohammed Issa 'Banka' akiingia JNIA leo asubuhi tayari kwa safari
    Kipa wa Simba SC, Beno Kakolanya akiwaongoza wenzake kuingia JNIA
    Hapa ni wakati wakipata mlo wa asubuhi kabla ya safari yao



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS WALIVYOONDOKA LEO DAR KUIFUATA BURUNDI KWA MECHI YA KUFUZU KOMBE LA DUNIA KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top