• HABARI MPYA

    Thursday, September 26, 2019

    MAN UNITED YASONGA MBELE KWA USHINDI WA MATUTA CARABAO CUP

    Wachezaji wa Manchester United wakipongezana baada ya ushindi wa penalti 5-3 kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya Rochdale kwenye mchezo wa Raundi ya Tatu Kombe la Ligi England usiku wa jana Uwanja wa Old Trafford. Manchester United ilitangulia kwa bao la Mason Greenwood dakika ya 68, kabla ya Luke Matheson kuisawazishia Rochdale dakika ya 76. Waliofunga penalti na Man United ni Juan Mata, Andreas Pereira, Fred, Greenwood na Daniel James wakati za Rochdale zilifungwa na Calvin Andrew, Aaron Morley na Aaron Wilbraham huku Jimmy Keohane pekee akikosa 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YASONGA MBELE KWA USHINDI WA MATUTA CARABAO CUP Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top