• HABARI MPYA

    Friday, September 20, 2019

    NDIKUMANA AREJEA MAZOEZINI AZAM FC IKIJIANDAA KUWAFUATA TRIANGLE UNITED MARUDIANO ZIMBABWE

    Mshambuliaji wa Azam FC, Mrundi Suleiman Ndikumana aliyekuwa majeruhi akifanya mazoezi na wenzake leo kuelekea mchezo wa marudiano wa Raundi ya Pili Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Triangle United Septemba 28 mjini Bulawayo, Zimbabwe 
    Beki David Mwantika akiuwahi mpira katka mazoezi kuelekea mchezo huo ambao Azam FC wanatakiwa kushinda 2-0 ugenini ili wasonge mbele, baada ya kuchapwa 1-0 nyumbani 
    Mshambuliaji Muivory Coast, Richard Ella 'Djodi akionyesha ustadi wake mkubwa katika kuumiliki mpira
    Mshambuliaji Mzambia, Obrey Chirwa akiwa mazoezini leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi 
    Mshambuliaji mwingine Mrundi, Emmanuel Mvuyekure akiondoka na mpira dhidi ya Masoud Ally 'Cabaye'
    Kiungo mshambuliaji, Iddi Kipagwile akielekeza jambo mazoezini 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NDIKUMANA AREJEA MAZOEZINI AZAM FC IKIJIANDAA KUWAFUATA TRIANGLE UNITED MARUDIANO ZIMBABWE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top