• HABARI MPYA

    Monday, March 27, 2017

    ENGLAND YAENDELEA KUTAWALA KUNDI F KUFUZU KOMBE LA DUNIA, YAIPIGA 2-0 LITHUANIA

    Jermain Defoe (kulia) akishangilia na mchezaji mwenzake, Raheem Sterling aliyemtilia krosi kuifungia England bao la kwanza dakika 21 katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Lithuania usiku wa jana Uwanja wa Wembley, London, England kwenye mchezo wa Kundi F kufuzu Kombe la Dunia. Mshambuliaji Jamie Vardy naye akatokea benchi kwenda kuifungia bao la pili England dakika ya 65 na kwa ushindi huo, Simba Watatu wanaendelea kuongoza kundi hilo kwa kufikisha pointi 13 baada ya kucheza mechi tano, wakifuatiwa na Slovakia wenye pointi tisa, Slovenia pointi nane, Scotland pointi saba, Lithuania pointi tano na Malta ambao hawana pointi PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ENGLAND YAENDELEA KUTAWALA KUNDI F KUFUZU KOMBE LA DUNIA, YAIPIGA 2-0 LITHUANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top