• HABARI MPYA

    Wednesday, December 02, 2015

    NI RWANDA NA SUDAN, UGANDA NA ETHIOPIA NUSU FAINALI ALHAMISI

    MABINGWA watetezi, Kenya wamevuliwa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challege baada ya kufungwa na Rwanda kwa penalti 5-3 kufuatia sare ya 0-0 mjini Addis Ababa, Jumanne.
    Amavubi sasa itakutana na Sudan katika Nusu Fainali, ambayo jana iliitoa Sudana Kusini kwa penalti 5-3 pia baada ya sare ya 0-0.
    Ikumbukwe Robo Fainali za kwanza Jumatatu, Uganda iliitoa Malawi kwa kuichapa mabao 2-0, wakati Ethiopia iliitoa Tanzania kwa kuifunga penalti 4-3 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 90. Nusu Fainali zinatarajiwa kuchezwa Alhamisi, Uganda ikimenyana na wenyeji Ethiopia na Rwanda ikivaana na Sudan. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI RWANDA NA SUDAN, UGANDA NA ETHIOPIA NUSU FAINALI ALHAMISI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top