• HABARI MPYA

    Wednesday, April 08, 2015

    TFF YAMPONGEZA TENGA

    Rais wa TFF, Jamal Malinzi (kushoto) na Leodegar Tenga kulia
    RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jamal Malinzi, amempongeza Leodgar Tenga kwa kuchaguliwa kuendelea kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
    Aidha Rais Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa wajumbe  waliochaguliwa kuwa wajumbe wapya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu baranai Afrika (CAF) na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).
    Katika salamu hizo na nakala zake kutumwa kwa Rais wa CAF, Issa Haytou na Rais wa FIF, Blatter, Malinzi amewatakia kila la kheri katika majukumu hayo mapya,na  kwa ajili ya maendeleo ya mpira wa miguu duniani.
    Tenga amechaguliwa nafasi hiyo baada ya kuwa mgombea pekee kutoka kanda ya Afrika Mashariki aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo na kuungwa mkono na nchi zote wanachama wa CECAFA.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF YAMPONGEZA TENGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top