• HABARI MPYA

    Wednesday, April 08, 2015

    STARS YAPANGWA NA NIGERIA, MISRI CHAD KUFUZU AFCON 2017

    Na Mwandishi Wetu, CAIRO
    TANZANIA imepangwa Kundi G pamoja na Nigeria, Misri na Chad katika michuano ya kuwania kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2017 nchini Gabon.
    Droo ya michuano hiyo imepangwa leo mjini Cairo, Misri.
    Gabon imezipiku Ghana na Algeria kushinda uenyeji wa AFCON ya 31.  Gabon walikuwa wenyeji washirika wa michuano hiyo mwaka 2012 pamoja na jirani zao, Equatirial Guinea.
    Makundi ya kufuzu AFCON 2017 yapo hivi; Kundi A; Tunisia, Togo, Liberia na Djibouti. Kundi B; DRC,  Angola, Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) na  Madagascar. Kundi C; Mali, Equatorial Guinea, Benin na Sudan Kusini.

    Kundi D lina timu za Burkina Faso, Uganda, Botswana na Comoros. Kundi E; Zambia Kongo, Kenya na Guinea Bissau. Kundi F, Cape Verde, Morocco, Libya na Sao Tome.
    Kundi G; Nigeria, Misri, Tanzania na Chad. Kundi H; Ghana, Msumbiji, Rwanda na Mauritius. Kundi  I; Ivory Coast, Sudan, Sierra Leone na Gabon. Kundi J; Algeria, Ethiopia, Lesotho na Shelisheli.
    Kundi K; Senegal, Niger, Namibia na Burundi, Kundi L; Guinea, Malawi, Zimbabwe na Swaziland. Kundi M; Cameroon, Afrika Kusini, Afrika Kusini, Gambia na Mauritania.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: STARS YAPANGWA NA NIGERIA, MISRI CHAD KUFUZU AFCON 2017 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top