• HABARI MPYA

    Saturday, May 01, 2021

    KAI HAVERTZ APIGA ZOTE MBILI CHELSEA YAICHAPA FULHAM 2-0

    MABAO ya kiungo Mjerumani, Kai Havertz dakika ya 10 na 49 yameipa Chelsea ushindi wa 2-0 dhidi ya Fulham katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London leo.
    Kwa ushindi huo, The Blues wanafikisha pointi 61 baada ya kucheza mechi 34, ingawa wanabaki nafasi ya nne wakizidiwa pointi mbili na Leicester City, wakati Fulham inayobaki na pointi zake27 za mechi 34 inasalia nafasi ya 18 ikizidiwa pointi tisa na Newcastle United.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAI HAVERTZ APIGA ZOTE MBILI CHELSEA YAICHAPA FULHAM 2-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top