• HABARI MPYA

    Saturday, May 29, 2021

    TANZANIA YAKAMILISHA MECHI ZAKE KWA KUCHAPWA 4-2 NA MISRI FAINALI ZA SOKA LA UFUKWENI NCHINI SENEGAL

     TANZANIA imeambulia kipigo cha mabao 4-2 mbele ya Misri katika mchezo wa kuwania nafasi ya tano kwenye Fainali za Afrika za soka la Ufukweni katika ufukwe wa Sally Beach, pembezoni mwa Bahari ya Atlantic Jijini Dakar, Senegal.
    Tanzania imekamilisha mechi zake za michuano hiyo bila kushinda hata moja kufuatia kufungwa 4-3 na Uganda na 3-1 na wenyeji, Senegal katika Kundi A.
    Fainali ya michuano hiyo inafanyika leo baina ya Senegal na Msumbiji, ambayo itatanguliwa na mechi ha kusaka mshindi wa tatu baina ya Morocco na Uganda.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA YAKAMILISHA MECHI ZAKE KWA KUCHAPWA 4-2 NA MISRI FAINALI ZA SOKA LA UFUKWENI NCHINI SENEGAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top