KLABU ya Yanga imeipongeza Azam Media Limited kwa kusaini mkataba mpya mnono na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wa Haki za Matangazo ya Televisheni ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Pamoja na Yanga, wafadhili na wadhamini wao, GSM kupitia Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Gharib Mohamed nao wameipongeza Azam Media kwa kitendo hicho.
Wiki hii Azam Media Limited imesaini mkataba mpya na TFF wa kuonyesha mechi za Ligi Kuu kwa miaka 10 zaidi kuanzia msimu ujao wenye thamani ya Sh. Bilioni 225.6.
0 comments:
Post a Comment