• HABARI MPYA

    Sunday, May 09, 2021

    INTER MILAN WAENDELEZA UBABE ITALIA, WAIPIGA SAMPDORIA 5-1

    TIMU ya Inter Milan imeichapa Sampdoria 5-1 Uwanja wa Giuseppe Meazza Jijini Milan na kuupendezesha ubingwa wake wa Ligi Kuu ya Itali, maarufu kama Serie A.
    Kwa ushindi huo, Inter Milan inafikisha pointi 85, 10 zaidi ya Napoli inayofuatia baada ya wote kucheza mechi 35.
    Inter Milan imekifikisha mechi 19 bila kupoteza na unakuwa ushindi wa 14 mfululizo nyumbani hiyo ikiwa ni rekodi kwa Nerazzurri, waliotwaa ubingwa wiki iliyopita zikiwa zimebaki mechi nne.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: INTER MILAN WAENDELEZA UBABE ITALIA, WAIPIGA SAMPDORIA 5-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top