• HABARI MPYA

    Saturday, July 04, 2015

    YATAKA MOYO KUMPA WEMA SEPETU UBUNGE!

    Na Hemed Kivuyo, DAR ES SALAAM
    BINADAM tumetofautiana sana tena sana, ni kama Mbingu na Ardhi, wakati mwingine anawaza adhana italia saa ngapi akasali, mwingine anawaza usiku utaingia muda gani akanywe pombe na kutembea uchi.
    Wakati mwingine anawaza ni namna gani abadili mbinu za kumwabudu Mungu, mwingine anawaza  avae nguo gani itakayomrahisishia kujiuza vizuri. Tumwachie Mungu.
    Hivi karibuni nilisikia taarifa kuwa mmoja kati ya wasanii wanaodaiwa kuwa na ‘sifa chafu’ nchini, Wema Sepetu ana nia ya kuwania ubunge kupitia viti maalum.
    Sijasikia atawania kwa Tiketi ya chama gani, lakini ina yoonekana ni CCM, kwa sababu amekuwa akionekana na ‘jezi’ za chama hicho.
    Mara baada ya kusikia taarifa hizo nilitafuta historia ya dada huyo kwa kuwa sikuwa namfahamu vizuri sana.
    Katika utafutaji huo wa historia yake nikakuta sifa zake nyingi ni ‘chafu’, wakati dhana ya uongozi ni kuonyesha njia, kuwa na busara na uwezo wa kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii inayokuzunguka.
    Wema aliwahia kupanda jukwaani na kuonyesha maungo yake, Waandishi wa Habari wakampiga picha na kwenda kuzichapisha gazetini
    Siku ya pili akaenda kulia kwa Waandishi wa Habari akijutia picha zilizochapishwa gazetini

    Kiongozi unapaswa kujiheshimu kabla hujaheshimiwa na ndiyo maana Mwalimu Nyerere aliwahi kutoa mfano juu ya Waziri mmoja huko Ulaya kufukuzwa baada ya kukutwa akitembea na mama mmoja wa barabarani.
    Uongozi siyo sifa tu kuitwa kiongozi, ni lazima uwe na busara na kuitumia katika utatuzi wa matatizo ya wananchi kwa kutumia akili, busara na hekima zaidi.
    Wakati natafuta historia ya mwanadada huyo, sikukuta sifa hata moja aliyonayo ambayo kiongozi anapaswa kuwa nayo. Nilikuta anamiliki sifa nyingi zisizofaa mbele ya jamii, zisizofaa kuigwa na kizazi chochote hapa Tanzania na sijui chama gani kitakubali `kujilipua’ kwa kumpa mzigo wa uongozi.
    Niliambiwa kuna wakati alipanda jukwaani akiwa amelewa na kuacha maungo yake wazi. Nikaambiwa alikuwa na mwenzake ambao baada ya pombe kuwaisha vichwani, wakawatafuta Waandishi wa Habari na kusimama mbele yao wakiomba radhi kwa kitendo hicho. 
    Mbunge mtarajiwa Wema Sepetu katika pozi la kimahaba

    Huyo ni Mbunge mtarajiwa wa CCM. Inataka moyo kusahau ‘uchafu’ wake wote ni na  kumpa dhamana ya chama aende bungeni.
    Nikaambiwa pia amekuwa na mahusiano ya `kingono` na wanaume tofauti tofauti, wengi wao wasanii wenzake na wafanyabiashara.
    Mara Nyingi anapokuwa katika shughuli mbalimbali iwe usiku au mchana, huonekana amevalia mavazi yasiyo ya kistaarabu.
    Katika mitandao mbalimbali ya kijamii picha zake huonekana akiwa na himaya ya mahaba na mwanaume au yeye mwenyewe akiwa katika hisia za mahaba kwa maana ya uchi ama nusu uchi. CCM wameingia katika mtego wa kumpa dhamana ya kuwawakilisha Bungeni kupitia viti maalum. Inataka moyo!

    (Mwandishi wa makala haya ni mtangazaji wa Redio One na ITV, ambaye anapatikana kwamba namba +255 655 250 157 na +255 752 250 157)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YATAKA MOYO KUMPA WEMA SEPETU UBUNGE! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top