• HABARI MPYA

    Sunday, July 26, 2015

    MAN UNITED YAICHAPA BARCELONA 3-1 MAREKANI

    MANCHESTER United imeichapa mabao 3-1 Barcelona katika mchezo wa kirafiki ziara ya kujiandaa na msimu Uwanja wa Levi mjini Santa Clara, Marekani.
    Wayne Rooney aliifungia bao la kwanza Manchester United dhidi ya mabingwa hao wa Ulaya dakika ya nane, kabla ya Jesse Lingard kuifungia bao la pili timu ya Louis van Gaal dakika ya 65.
    Mabao mawili yakafungwa ndani ya dakika moja, ya 90, Barcelona wakianza kupitia kwa Rafinha kanla ya Adnan Januzaj kuifungia United bao la tatu.
    Kikosi cha Man Utd kilikuwa; de Gea/Johnstone dk62, Darmian/Valencia dk62, Jones/Smalling dk62, Blind/McNair dk62, Shaw/Blackett dk62, Carrick/Herrera dk62, Schneiderlin/Fellaini dk62, Mata/Perreira dk62, Depay/Lingaard dk62, Rooney/Januzaj dk62 na Young/Wilson dk62.
    Barcelona; Ter Stegen/Masip dk45, Adriano/Rakitic dk45, Piquet/Bartra dk68, Vermaelen/Matthieu dk60, Alba, Busquets/Gumbau dk68, Rafinha, Iniesta/Halilovic dk68, Sergi Roberto, Suarez/Sandro dk68 na Pedro/Munir dk68.
    Luis Suarez wa Barcelona (kulia) akifumua shuti mbele ya Daley Blind wa Manchester United PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YAICHAPA BARCELONA 3-1 MAREKANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top